July 16, 2015



Pamoja na maandalizi ya kambi mjini Lushoto, Simba wametumia muda wao mchache kutembelea kituo cha watoto yatima cha Irente.



Wakiongozwa na Kocha Dylan Kerr, Simba na kikosi chao kizima walitua katika kituo hicho kilichopo Lushoto pia na kuzungumza na watoto hao ikiwa ni pamoja na kuwaliwaza.

Kerr alionekana kufurahishwa na suala hilo na kusema lilikuwa jambo zuri.


“Kama watu wanaoaminika au wanaotazamwa na jamii, ni jambo jema kuungana na wanajamii wengine kama tulivyofanya,” alisema Kerr raia wa Uingereza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic