January 24, 2014



 
KIKOSI CHA TOTO MSIMU ULIOPITA
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA), wametoa muda kwa Klabu ya Toto Africans kufanya uchaguzi mwishoni mwa mwezi huu na kama wasipofanya hivyo, timu hiyo itashushwa daraja.


 Mwenyekiti wa MZFA, Jackson Songora amesema kuwa klabu hiyo imepewa muda kufikia mwishoni mwa mwezi huu lazima iwe imeshafanya uchaguzi, bila hivyo timu hiyo inaweza kushushwa daraja.

Songora alisema klabu hiyo imekuwa na mivutano ambayo haina msingi na kusababisha pia kusuasua hata kwenye mechi zake za Ligi Daraja la Kwanza.

“Toto wanatakiwa kufanya uchaguzi kabla ya mwezi huu kumalizika, hatutaki kuona migogoro ya mara kwa mara ambayo inasababisha timu kufanya vibaya,” alisema Songora.
 SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic