Mshambuliaji wa zamani wa Simba,
Emmanuel Gabriel ametamba kuwa kikosi chake hicho cha zamani hakitatoka katika
mechi ya kesho.
Simba tayari iko mjini Mbeya
kuivaa Prisons katika mechi ya Ligi Kuu Bara na Gabriel maarufu kama Batigol
ametamba timu yake mpya itashinda.
“Najua Simba wana kikosi kizuri,
wala hatuwezi kubweteka kwa kuwa wamefungwa na Waangola.
“Lakini nakuhakikishia huku
hawatatoka, wakibahatisha ni sare. Kikosi chetu kiko fiti sana,” alisema
Gabriel.
Wakati Gabriel anatamba, Kocha
Mkuu wa Simba, Patrick Liewig anaamini watabadilika na kucheza vizuri.
“Tumeona makosa na tumeyafanyia
kazi, hofu kubwa ni ubovu wa kiwanja lakini tutafanya vizuri na kushinda.
“Timu kubwa kama Simba lazima
itakuwa inapaniwa, wachezaji wanalijua hilo na tutakuwa makini zaidi,” alisema
Mfaransa huyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment