Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), leo imekabidhi basi aina ya
Yutong kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya matumizi ya timu ya
soka ya taifa (Taifa Stars).
Stars ambayo siku za hivi karibuni iling’ara katika mechi za
kirafiki kwa kuzitwanga Zambia na Caneroon, itakuwa ikitumia basi hilo kubwa
aina ya Yutong lenye thamani ya Sh milioni 200.
Pamoja na basi hilo, TBL imeongeza udhamini wake kwa Stars na jumla itakuwa Sh bilioni 4.2 badala ya ile ya Sh bilioni 3.2 ya awali.
Pamoja na basi hilo, TBL imeongeza udhamini wake kwa Stars na jumla itakuwa Sh bilioni 4.2 badala ya ile ya Sh bilioni 3.2 ya awali.
TBL kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro ni wadhamini wa
Taifa Stars pia mabingwa wa soka Tanzania, Simba na vinara wa Ligi Kuu Bara,
Yanga ambao wote wameshakabidhiwa basi kama hilo.
Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye makao makuu ya TBL, Ilala
jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi kutoka TBL, TFF pamoja na Kocha
Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen.
0 COMMENTS:
Post a Comment