Amrouche
Kocha
Adel Amrouche raia wa Ubeligiji ndiye kocha mpya wa timu ya soka ya taifa ya
Kenya, Harambee Stars baada ya kupewa mkataba mpya.
Amrouche
ambaye asili yake ni nchini Algeria aliwahi kutaka kuinoa Taifa Stars baada ya
kuondoka kwa Maximo, hata hivyo juhudi zake ziligonga mwamba, kazi akapewa Jan Poulsen maarufu kama Babu.
Ntagwabira
Mbeligiji
huyo, naye amemtangaza Jean Marie Ntagwabira raia wa Rwanda ambaye aliwahi
kuitaka Yanga bila ya mafanikio kuwa kocha msaidizi.
Jean
Marie alikuwa kocha msaidizi wa Rwanda ‘Amavubi’ chini ya Mserbia, Sredojevich
Milutin ‘Micho’ wakati Amrouche aliamua kuvunja mkataba wake wa miaka mitano
kuinoa Burundi ‘Itamba Murugamba’.
Kenya
ambayo imeomba kuwa mwenyeji wa Kombe la Mataifa Afrika mwaka wa miaka 2019
imeamua kuingia mkataba na Amrouche ambaye alionyesha juhudi na uchapakazi
wakati akiwa na Burundi bila ya kujali shida na matatizo mengi katika kikosi
hicho.
Amrouche
amewapiku makocha zaidi ya 30 waliokuwa wanawania nafasi hiyo mara baada ya
Mfaransa, Henri Michel kuamua kuachia ngazi.
Kwa
upande wa klabu Amrouche aliwahi kung’ara na DC Motema Pembe ya DR Congo wakati
Jean Marie alifanya vizuri na APR na baadaye Atraco zote za Rwanda ambazo
alizipa ubingwa wan chi hiyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment