picha na saleh ally
Kocha Mkuu wa Recreativo Libolo amesema ni lazima waifunge Simba katika mechi ya marudiano ili kusonga mbele kwa kujiamini zaidi.
Akizungumza na mtandao wa Angolasports, Henrique Calisto
amesema ana uhakika wataishinda Simba na watafanya hivyo kuifanya timu yake
kuwa na uhakika zaidi.
“Ushindi unajenga hali ya kujiamini, bado Simba si timu ya
kudharau lakini tunataka kushinda na si are. Tukishinda tutajiamiani na zaidi
katika hatua inayofuata.
“Kitu kizuri kwetu ni kuishinda Simba itakapocheza nasi hapa
Angola. Ushindi wa Dar es Salaam, bado si majibu sahihi kwetu, tumemaliza
mchezo mmoja, sasa unafuata wa pili,” alisema Calisto.
Katika mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Libolo
iliibuka na ushindi wa bao 1-0 na kufanikiwa kuonyesha soka la kuvutia dhidi ya
wenyeji wake Simba.
Libolo ambao watakuwa wenyeji katika mchezo wa pili,
wanahitaji sare tu ili kusonga mbele, wakati Simba wanahitaji ushindi wa zaidi
ya mabao mawili halafu wasiruhusu hata bao moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment