MAMBO yanaweza yakaenda kuliko
yalivyotegemewa kwa Kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic kulipwa fedha
zake ndani ya saa 48, awali ilikuwa hadi Jumapili ndiyo malipo yangekuwa yamekamilika.
Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi
amethibitisha kwamba tayari yuko jijini Muscat, Oman na ameanza kulishughulikia
suala la Milovan.
“Huenda ikawa mapema zaidi, tayari
nimeanza kufanya mchakato, hadi leo mchana huu (Alhamisi) nitakuwa nimepiga
hatua.
“Ingawa nimebanwa na mambo yangu
mengine, lakini nitajitahidi kulimaliza ndani ya leo na kesho na kocha atakuwa
ameshapata fedha zake,” alisema Rahma ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa kamati
ya fedha ya Simba.
Malkia wa nyuki aliamua kuingilia na
kutangaza kumlipa Milovan fedha dola 32,000 anazowadai Simba ambazo zilitokana
na mishahara yake minne.
Tokea ametua nchini, hakuna kiongozi
hata mmoja wa Simba aliinua mguu wake na kumfuata kwa ajili ya mazungumzo.
Badala yake, wengi walikuwa wakimuona
Uwanja wa Taifa jijini Dar alipokuwa anakwenda kushuhudia mechi mbalimbali za ligi ikiwemo
ila kati ya Simba dhidi ya Libolo.
Katika mechi hiyo Mwenyekiti wa
Simba, Ismail Aden Rage alimfuata na kumyanyua mkono akionyesha wako pamoja
naye, lakini mashabiki wakamzomea.
0 COMMENTS:
Post a Comment