Baada ya kuamka na ushindi wa bao 1-0
dhidi ya wenyeji wao Prisons ya Mbeya jana, mabingwa wa soka Tanzania, Simba
wameamua kupasha ‘msuri’ kwa kubaki mjini humo.
Leo jioni, Simba itacheza mechi ya
kirafiki dhidi ya kikosi cha Mbeya City ambacho kimepanda daraja hadi Ligi Kuu
Bara msimu ujao.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri
Kihwelo amethibitisha Simba kubaki Mbeya na kucheza mechi ya kirafiki.
“Tumeamua kufanya mazoezi kidogo,
baada ya hapo tutaondoka kurudi Dar. Tunajua hii ni sehemu ya mazoezi nab ado kuna
makosa tunaendelea kurekebisha,” alisema Julio.
0 COMMENTS:
Post a Comment