February 23, 2013




Siku ya kumaliza ubishi imewadia, Yanga v FC Azam katika mechi ya Ligi Kuu Bara  kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu, leo ndiyo siku ya kumaliza ubishi, raha kila timu ina pointi 36 ingawa Azam wana mchezo mmoja zaidi waliocheza.
Ushindi ni kitu muhimu kwa kila upande, lakini kuna mengi ya kujiuliza kwamba itakuwa vipi?

TAKWIMU:
Takwimu zinaonyesha timu zote mbili hazina tofauti kubwa katika mambo mengi muhimu, mfano ukiangalia mechi za mwisho Yanga ilishinda 4-0 dhidi ya African Lyon na Azam FC ikashinda kwa idadi hiyo dhidi ya Ruvu JKT.
Yanga imeshinda mechi 11 na kupoteza mbili, ina sare tatu wakati Azam FC pia imeshinda 11, imepoteza tatu na sare tatu.

KUFUNGA&KUFUNGWA:
Yanga imefunga mabao 33 na kufungwa 12 na kuifanya safu yake ya ulinzi kuwa imara zaidi hadi sasa na Azam FC imefunga mabao 31 na kufungwa 14, unaweza kusema hata wao safu yao ya ulinzi bado ni imara.

VIUNGO:
Viungo wa timu zote mbili watakuwa kivutio leo, Yanga ikiwategemea zaidi Athuman Idd ‘Chuji’ na kiungo nyota kutoka Rwanda, Haruna Niyonzima. Lakini Azam FC wana Humphrey Mieno, Ibrahim Mwaipopo na kiungo mtaalamu wa Kitanzania, Salum Abubakari ‘Sure Boy’.

WASHAMBULIAJI:
Kila upande una washambuliaji hatari, John Bocco amerejea dimbani, ni mwiba mkali kwa Yanga lakini wana Mganda, Brayan Umonyi pamoja na makinda wawili hatari, Hamis Mcha na Seif Abdallah.
Kiongozi wa mashambulizi hayo atakuwa Kipre Tchetche raia wa Ivory Coast ambaye anaongoza listi ya wafungaji wa Ligi Kuu Bara kwa kuwa na mabao 10 akifuatiwa na 
Didier Kavumbagu wa Yanga mwenye tisa.

Yanga pia ina hazina ya watikisa nyavu kama Kavumbagu, Jerry Tegete, Said Bahanuzi na Hamis Kiiza na kocha wao, Ernie Brandts atakuwa na kazi ya kuchagua ingawa inaonekana lazima ataanza na Tegete ambaye sasa yuko ‘on fire’.

WAKONGWE:
Kila upande una wakongwe na hawapaswi kudharauliwa, Nizar Khalfan kwa Yanga na Gaudence Mwaikimba na Abdi Kassim ''Babi' kutoka Azam FC.
Bado ni wachezaji wenye uwezo na wakati mwingine wanakuwa bora zaidi katika mechi ngumu kama hizo.

Inawezekana kabisa, mwamuzi wa mechi ya leo analazimika kutulia zaidi ili adhibiti mchezo na kuondoa hisia kwamba kuna upande unaweza ukawa umecheza game hata kabla ya kuingia uwanjani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic