February 22, 2013




Pikipiki iliyobuniwa na mshambuliaji nyota wa Man United, Wayne Rooney imeuzwa kwa kitita cha pauni 43,000 (zaidi ya Sh milioni 90).
Pikipiki hiyo imebuniwa na Rooney mwenyewe baada Lauge Jensen raia wa Denmark kumshauri Rooney kufanya hivyo kwa ajili ya kuiza ili kusaidia mambo mbalimbali ya jamii hasa watoto wenye matatizo.

Hata hivyo, mauzo hayo ya pauni 43,000 ya pikipiki hiyo yenye kasi ya 155 kwa saa yalikuwa pungufu pauni 15,000 tofauti na makadirio ya awali.

Hata hivyo pikipiki hiyo iliyobuniwa na Rooney mwenye miaka 27, imekuwa kivutio kwa wengi na huenda zinaendelea kupata soko na kumsaidia kuingiza mamilioni hya fedha.
Wakati wa kubuni, Rooney alitumua mfano wa picha yake wakati akishangilia baada ya kufunga bao la tik-tak katika mechi dhidi ya wapinzani wao wakubwa Man City, mwaka 2001.

Katika tanki la mafuta, imewekwa picha ya namba 10 ambayo anavaa Rooney akiwa na Man United. Pia kuna mapambo 22 madogomadogo ambayo yamepakwa almasi na ‘madigadi’ yake imeandikwa WR10 ambayo ni utambulisho wa mchezaji huyo.
Inaaminika kilichosababisha pikipiki hiyo kununuliwa kwa bei ya chini ni Rooney kushindwa kuwashawishi wateja, kwani awali walitegemea inunuliwe kwa pauni 56,000 kwani mara nyingi pikipiki za Lauge Jensen zimekuwa zikinunuliwa hadi pauni 60,000.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic