March 12, 2013




Kocha wa Polisi Morogoro, Adolf Rishard ndiye ameng’ara zaidi katika mzunguko wa pili hasa mechi zilizochezwa mwishoni mwa mwezi uliopita na mwanzoni mwa mwezi huu.

Rishard aliyewahi kung’ara wakati akiwa mchezaji, ameiongoza Polisi Morogogo kushinda mechi tatu mfululizo ikiwa ni pamoja na kutoka sare na Azam FC kwa kufungana nayo bao 1-1.

Pamoja na kwamba Azam FC imekuwa ni mwiba kwenye Uwanja wa Chamazi Complex inaoumiliki, lakini kikosi cha Rishard kilionyesha ni imara na kupata sare hiyo.


Azam FC imekuwa hatari inapokuwa kwenda dimba hilo, kwani hivi karibuni pamoja na Mtibwa Sugar kuzisumbua Yanga na Simba katika mechi nne ilizocheza nazo bila ya kupoteza hata moja, ilijikuta ‘ikilamba’ bao 4-0 kutoka kwa Azam kwenye uwanja huo.

Wakati Polisi Moro inaonkena inapigania maisha kutokana na kuwa mkiani, lakini iliweza kupata sare hiyo huku ikionyesha soka ya kuvutia chini ya uongozi wa kocha huyo msaidizi wa zamani wa Twiga Stars.

Polisi Moro imeshinda mechi tatu tu baada ya kucheza 20, imefunga mabao 10 na kufungwa 19 huku ikiwa pointi 17 katika nafasi ya 12 kati ya timu 14 za ligi hiyo. 

Rishard alitua Polisi Moro kuchukua nafasi ya mkongwe mwingine, John Simkoko baada ya kuingoza timu hiyo mechi 13 za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara bila ya ushindi hata mmoja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic