March 12, 2013




Beki matata wa Barcelona, Dani Alves amewashukia mashabiki wa wapinzani wao Real Madrid na kusema hajali hata kidogo chuki zao.

Alves ameliambia jarida maarufu la El Mundo kuwa, wala hajawahi kukosa usingizi kutokana na kuchukiwa na mashabiki wa Madrid kwa kuwa angekuwa anachezea timu hiyo, huenda wale wa Barcelona pia wangemchukia.

“Ni kitu cha kawaida kabisa, kamwe siwezi kuinua mdomo kuwaomba wasinichukie. Wanajua wanachokifanya nami naijua kazi yangu.

“Inawezekana hata wa Barcelona wangeweza kunichukia kama ningekuwa nachezea Real Madrid, ukiangalia vizuri ndiyo mambo ya soka,” alisema alves raia wa Brazil.
Alipoulizwa kuhusiana na Barcelona kupoteza mvuto kama ilivyokuwa awali hasa kuhusiana na uchezaji wake.


Alves alikiri kuwa na mabadiliko na Barcelona kutocheza soka lake, lakini akasisitiza tayari kikosi chao kimerejea katika kiwango chake na itaanza kuonyesha makali katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya AC Milan, baada ya kuwa imelala kwa mabao 2-0 ugenini nchini Italia katika mechi ya kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic