March 12, 2013



Okwi, wa tatu kushoto akiwa mazoezini na kikosi cha Etoile du Sahel, juzi..
 Simba imepanga kutuma wajumbe nchini Tunisia kwenda kufuatilia malipo ya kiungo mshambuliaji wake wa zamani, Emmanue Okwi.

Wanachotaka Simba ni kulipwa fedha zao dola 300,000 au warudishiwe Okwi na tayari wamepeleka maombi yao kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuhusiana na hilo.
Lakini rafiki wa karibu wa Okwi, amesema kamwe Mganda huyo hatakubaliana na hilo la kurejea nchini na kuichezea Simba, badala yake wao ndiyo wamalizane na klabu yake mpya ya Etoile du Sahel.


“Tayari Okwi anajua kila kitu, lakini kaniambia kamwe hawezi kuthubutu kurejea Tanzania kwa kuwa alishamalizana vizuri na Simba pamoja na Etoile du Sahel ambayo ilimlipa fedha yake.

“Hivyo anaona ni vizuri aendelee kubaki hapo huku akijaribu kupambana na maisha,” alisema rafiki huyo.

Pamoja na rafiki yake huyo kusema hiyo, inaonekana ni vigumu kwa Okwi iliyeelezwa analipwa mshahara wa dola 15,000 kurejea nchini kuchukua dola 1,200 aliyokuwa akilamba Simba.

Okwi bado hajapata namba katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo, lakini amekuwa akiendelea mazoezi na wenzake wa kikosi cha kwanza huku akionekana kuwa na nyuso ya furaha.

Etoile du Sahel iliahidi kuilipa Simba fedha hizo za usajili kwa mafungu mawili, lakini haikutekeleza suala hilo na imekuwa ikiendelea kupiga kalenda.

Imeelezwa, Simba wamemuomba Malkia wa Nyuki ambaye ni mlezi wao, kupanda hadi Tunisia kwenda kulishughulikia suala hilo badala ya kuwaamini Fifa ambao wakati mwingine wamekuwa wazito kushughulikia matatizo ya timu zisizokuwa maarufu sana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic