April 16, 2013





Mrembo Fanny Neguesha ameamua kuonyesha wazi penzi lake kwa mwasoka mtukutu, Mario Balotelli kwa kuchora tatuu inayomhusu.

Mwanamitindo huyo wa Ubeligiji amechora alama inayoonyesha ana furaha na penzi lake kwa Balotelli.


Neguesha ameandika ujumbe huo katika mkono wake wa kushoto kwa ndani na inaelezwa waliongozana pamoja.

Pamoja na tatuu hiyo ya kuonyesha penzi lake kwa Balotelli, Fanny ,22, pia amechora ramani ya Afrika shingoni mwake.

Balotelli aliyejiunga na AC Milan akitokea Man City kwa dau la pauni milioni 19 amekuwa akifanya vizuri baada ya kufunga mabao nane katika mechi tisa alizocheza.

Lakini penzi lake na Fanny limekuwa gumzo zaidi na wamekuwa wakionekana pamoja sehemu mbalimbali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic