April 17, 2013





Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig amegoma kurudishwa kikosini kwa wachezaji wakongwe wakiwemo Haruna Moshi Boban na Amir Maftah.

Kocha huyo raia wa Ufaransa ameuambia uongozi kwamba anataka kumaliza msimu akiwa na kikosi cha wachezaji alionao, wengi wakiwa makinda.

Mfaransa huyo ambaye tokea ajiunge na Simba imekuwa ikienda mwendo wa kusuasua, tayari amewasilisha ripoti yake kwa uongozi kueleza kusimamishwa kwa wachezahji hao kwa utovu wa nidhamu.

Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amethibitisha Liewig kuwasilisha ripoti yake kuhusiana na wachezaji hao.

Wachezaji wengine waliosimamishwa ni pamoja na Juma Nyosso, Abdallah Juma na Paul Ngalema.


Uongozi wa Simba umesema utalijadili suala hilo na kujua kama kuna kitu cha kufanya au la.

Liewig amekuwa akilaumiwa na wachezaji wengi kutokana na tabia yake ya kuwanunia wachezaji hasa wanapokuwa wamekosea.

Badala ya kumalizana nao, Liewig amekuwa akinuna na kutotaka wachezaji hao wasijumuike katika kikosi, kitu ambacho baadhi yao wamekuwa wakilaumu na kusisitiza ingekuwa jambo la busara kama kocha huyo angekuwa akiwaita na kutatua kinachosababisha mgongano.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic