April 18, 2013





 
CHELSEA V FULHAM

Chelsea ikiwa nyumbani ilionyesha kiwango baada ya kuichapa Fulham kwa mabao 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu England kwenye Uwanja wake wa Stamford Brigde maarufu kama Darajani.
 


 Kitu kizuri zaidi kwa Chelsea, mabao yake yote matatu yalifungwa na mabeki wake wa kati.

Luiz raia wa Brazil alifunga bao katika dakika ya 30 na nahodha John Terry akaongeza la pili katika dakika ya 43 na timu zikaenda mapumziko, Chelsea ikiwa mbele kwa mabao hayo mawili.


Mara kadhaa katika kipindi cha pili, washambuliaji wa Chelsea, Moses na Torres walipoteza nafasi kadhaa ambazo zingezaa mabao.

Chelsea ambayo imefudi katika nafasi ya tatu baada ya kufikisha pointi 61, ikiwa ni moja zaidi ya Arsenal, ilipata bao lake la tatu katika dakika ya 71 baada ya Terry kuunganisha pasi ya kichwa kutoka kwa Torres.


  
MAN CITY V WIGAN
Manchester City ikiwa nyumbani ilifanikiwa kushinda kwa bao 1-0 dhidi ya Wigan ambao walionyesha ni wabishi kuanzia mwanzo.
City walipata bao lao hilo katika dakika ya 83 mfungaji akiwa Carlos Tevez.
Pamoja na bao hilo, City waliendelea kufanya kazi ya ziada kwani Wigan walionyesha kiwango kizuri na kuwapa wakati mgumu mabingwa hao watetezi.
 
WEST HAM V MAN UNITED
Pamoja na kuwa katika mbio za ubingwa, Man United ikiwa ugenini ilijikuta ikiwa katika wakati mgumu sana dhidi ya wenyeji wake West Ham.


West Ham walianza kufunga bao mapema kupitia Vaz Te katika dakika ya 16, lakini Valencia akaisawazishia Man United katika dakika ya 31 na matokeo hayo yakadumu hadi mapumziko.


Kipindi cha pili, Diame aliipatia bao West Ham katika dakika ya 55 na Man Unite wakasawazisha kupitia van Persie katika dakika ya 76 ingawa bao hilo lilielezwa kuwa ni offside.


Picha zinaonyesha kabla ya kufunga bao hilo, van Persie alikuwa mbele ya mabeki wa West Ham, hivyo alikuwa ameotea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic