April 13, 2013



Hakuna ubishi tena kwamba ushindi wa leo wa Yanga wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Oljoro umeivua Simba ubingwa wa Tanzania Bara.

Simba iliyojaa migogoro, ina pointi 35 na michezo mitano ukiwemo wa kesho dhidi ya Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.


Iwapo Simba itashinda mechi zake zote tano, ina uwezo wa kufikisha pointi 50 wakati tayari Yanga imefikisha 52.

Maana yake, Simba inaweza kugombea nafasi ya pili iwapo haitapoteza mechi ya kesho. Kama itafungwa na Azam pia itakuwa ni wiki ngumu kwake kwa kuwa itakuwa imeondolewa tena kuwania nafasi ya pili.

Azam ikishinda itafikisha pointi 49, wakati Simba itakayokuwa imebakiza michezo minne, ikishinda yote itakuwa na 47.

Simba chini ya Ismail Aden Rage imeandamwa na migogoro ikiwa ni pamoja na baadhi ya viongozi kujiuzulu.

Hivi karibuni ilimtimua kocha wake, Milovan Cirkovic ambaye amerejea kwa Serbia na kumpa nafasi Mfaransa, Patrick Liewig ambaye kikosi chake kimekuwa kikisua.

Pia Simba imeingia mgogoro na wachezaji wake wengi wakongwe ingawa tayari Felix Sunzu na Mwinyi Kazimoto waliokuwa wamondolewa kikosi kama ilivyo kwa akina Haruna Moshi, Ramadhani Chombo, wamerudishwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic