April 13, 2013








Full time:
MPIRA UMEKWISHAAAAAAA
Dk 90*2, kipa Ally Mustapha wa Yanga anafanya kazi ya ziada kuokoa shuti la Majaliwa Sadick, inakuwa kona lakini ambayo haikuzaa matunda.
Dk 89, Bahanuzi anainua mpira juu, pamoja na kumpita kipa lakini unakwenda pembeni ya lango. Juhudi za Kiiza kuuwahi zinashindwa kuzaa matunda.

 
Dk 83 Yanga wanafanya shambulizi ambalo halikuzaa matunda baada ya krosi nzuri ya Nizar kutua kwa Kiiza lakini hakuwa makini


Dk 79, Yanga inamtoa Msuva anaingia Nizar Khalfan
Dk 59-63 Yanga inatumia muda mwingi kwa kupiga pasi za shoo huku mashabiki wake wakishangilia kwa nguvu.


Dk 57, Yanga inalazimika kufanya mabadiliko kwa kumtoa Bahanuzi baada ya kugongana na kipa wa Oljoro, anaingia Said Bahanuzi.


Dk 50, Oljoro wanamtoa kipa Mussa Lucheke, anaingia Shaibu Issa


HALF TIME YANGA 3-OLJORO 0
GOOOOO dk 43, Yanga wanaachiana pasi maridadi na mwisho Kiiza anakimbia na mpira na kumchambua kipa wa Oljoro kuandika bao la tatu.
 
Dk 32, Yanga inamtoa Juma Abdul aliyeumizwa na Idd Saleh na nafasi yake ya beki wa kulia inachukuliwa na mkongwe, Shadrack Nsajigwa ambaye alikuwa akishangiliwa sana na mashabiki wa Yanga wakati akipasha misuri.

Dk 24, Kavumbagu anashindwa kufunga baada ya kupokea pasi nzuri ya Msuva akiwa katika nafasi nzuri ya kuipatia Yanga bao la tatu.


 Dk 24, Kavumbagu anashindwa kufunga baada ya kupokea pasi nzuri ya Msuva akiwa katika nafasi nzuri ya kuipatia Yanga bao la tatu.



GOOOOO Dk 19, viungo wa Oljoro wanapoteza mpira na Msuva anauchukua, anawakimbiza mabeki wanne wa Oljoro na kuandika bao la pili kwa shuti kali.
Dk 15, Oljoro wanajaribu kupeleka shambulizi langoni mwa Yanga, hata hivyo wanaonekana kuwa dhaifu na wasio na madhara.
Dk 14, Shambulizi kali katika lango la Oljoro, krosi murua ya Kiiza inamkuta Msuva lakini shuti lake linapaa sentimeta chache juu ya goli.



Dk 7, Yanga wanaendelea kufanya mashambulizi mfululizo huku mabeki na viungo wa Oljoro wakiwa wamerudi nyuma.

GOOOOO dk 5 anafunga kwa kichwa baada ya kona iliyochongwa na Niyonzima.

Dk 3, Yanga wanaanza na shambulizi kali langoni mwa Oljoro, shuti kali la Msuva linapanguliwa na kipa na kuwa kona.
  Vikosi vimerudi vyumbani, tayari kwa ajili ya kuanza mechi.
KIKOSI CHA YANGA LEO:
1.Ally Mustafa 'Barthez' 2.Juma Abdul 3.David Luhende 4.Nadir Haroub 'Cannavaro' 5.Kelvin Yondani 6.Athuman Idd 'Chuji' 7.Simon Msuva 8.Frank Domayo 'Chumvi' 9.Didier Kavumbagu 10.Hamis Kiiza na 11.Haruna Niyonzima

Subs: 1.Yusuph Abdul 2.Shadrack Nsajigwa 3.Oscar Joshua 4.Salum Telela 5.Nurdin Bakari 6.Nizar Khalfani na 7.Said Bahanuzi

1 COMMENTS:

  1. Big Up Salehe kwa live show yako...umetusaidia sana wa ughaibuni tuliokua na hamu ya kufuatilia mtanange wa uamuzi wa nani atakua bingwa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic