May 5, 2013



 Borussia Dortmund na Bayern Munich zimekutana katika mechi yao ya Ligi ya Ujerumani, Bundesliga na kutoka sare ya bao 1-1 lakini vituko vingi vikatawala.

Mechi hiyo imechezwa jana Jumamosi, kivutio zaidi ilikuwa ni namna makocha wa timu hizo walivyobadili vikosi vyao ikiwa ni pamoja na kupanga wachezaji wengi wageni.


Hali hiyo inatokana na kwamba, timu hizo ndiyo zilizoingia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakayopigwa Mei 25 kwenye Uwanja wa Wembley jijini London, England.

Dortmund iliyokuwa nyumbani ilichezesha wachezaji sita tu wa kikosi cha kwanza wakati wageni Bayern wakachezesha wacheza watatu tu wa kikosi cha kwanza.


Dortmund maarufu kama BVB waliwapumzisha Sven Bender, Mats Hummels, Lukasz Piszczek na Marco Reus. Ilkay Gündagon akatolewa katika dakika ya 13 tu wakati wageni wao Bayern waliwapumzisha Arjen Robben, Bastian Schweinsteiger, Dante, Philipp Lahm, Javi Martinez, Thomas Müller, Mario Mandzukic na Franck Ribery

Wakati mechi inaendelea taarifa zikaeleza kiungo mkongwe Schweinsteiger na Robben waliungana na Rais wa klabu yao, Uli Hoeneß mjini Munich kuangalia mechi ya mpira wa kikapu kati ya Bayern Munich dhidi ya ALBA Berlin.

Katika mechi hiyo BVB walipata bao lao mapema tu baada ya Nuri Sahin kupiga pasi ndefu kwa Jakub Blaszczykowski aliyepiga krosi nzuri iliyomkuta Kevin Großkreutz aliyefunga bao matata na kumuacha kipa Manuel Neuer akiwa amezubaa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic