May 5, 2013

 
Floyd Mayweather amerudi ulingoni na kufanikiwa kushinda pambano lake la kwanza akitokea jela. Ameshinda kwa pointi 117-111, 117-111 na 117-111.


Mayweather amemshinda Roberto Guerrero kwa pointi katika pambano la raundi 12 ambalo alilitawala kwa karibu raundi zote tokea mwanzo katika pambano hilo lililofanyika katika Ukumbi wa MGM Grand jijini Las Vegas.


Pambano hilo lilikuwa ni la kuwania mkanda wa WBC katika  welterweight na sasa welterweight amefikisha mapambano 45 bila ya kufikisha.

Mayweather alikuwa akimpiga Guerrero ngumi za kushtukiza hali iliyomfanya wakati mwingine achanganyikiwe.



Kazi ya Mayweatherilikuwa ni kupiga ngumi na kutoka haraka, wakati Guerrero alipoteza ngumi nyingi sana kutokana na umahiri wa mpinzani wake wa kukwepa.


Mayweather amerejea ulingoni mara ya kwanza ikiwa miezi 12 tokea apigane pambano lake la mwisho pia ni mara yake ya kwanza kuzichapa ulingoni baada ya kuwa ametoka jela alikokumbana na kifungo cha miezi miwili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic