May 28, 2013




Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ametua jijini Barcelona kwa lengo la kula bata tu, akiwa ameongozana na mkewe.

Brandts raia wa Uholanzi ameiambia Salehjembe kwamba ameamua kwenda Barcelona kwa ajili ya kubadili mazingira.

Lakini pamoja na hivyo, ametaka kula bata akiongozana na mkewe ili awe kamili atakaporejea nchini kuanza maandalizi.
“Nitakaa hapa kwa siku kadhaa kabla ya kurejea Uholanzi, niliona hapa ni sehemu nzuri ya kubadili mazingira.


“Narudi Dar mwanzoni mwa mwezi ujao, lakini hapa nimebakiza siku tatu kabla ya kurudi nyumbani,” alisema Brandts.
Msimu huu, Brandts ambaye amejiunga na timu hiyo akitokea APR ya Rwanda, amefanikiwa kuipa ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Pamoja na hivyo ameiwezesha kulipa kisasi kwa kuifunga Simba mabao 2-0 katika mechi ya kufunga msimu. 

Hata hivyo, mashabiki wa Simba wamekuwa wakikubali kufungwa na watani wao lakini wakisisitiza bado hawajalipa ukubwa wa kipigo cha mabao 5-0 walichokipata Yanga katika mechi ya mwisho kufunga msimu uliopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic