May 3, 2013




Mashabiki wa Yanga wamekuwa wakilalama kwamba Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig ana shati moja tu la rangi nyeupe.
 
Mbaya zaidi wamekuwa wakisonga mbali zaidi kwa kudai shati la kocha huyo halijapimwa saizi na halimtoshi.


Mfano wao ni kwamba akichomekea linatokelezea vibaya, hivyo huenda anapaswa kushauriwa.

Salehjembe ilimhoji mara moja, jibu la Liewig liliwa hili: “Sijaja kuzungumzia shati au mavazi, kama hauvutiwi na nilichovaa shauri yako, mimi sijali.”

Lakini katika mechi kati ya Simba dhidi ya Polisi Moro, ‘mtu mzima’ Liewig alitoka kivingine na kuwafunga midogo mashabiki wa Yanga.
Safari hii alipiga ‘pensi’ safi nyeupe akiachia mguu kidogo, halafu akapiga raba kali ya chata kubwa ya Nike.

Raba hiyo ilikuwa ‘ikimechisha’ kitu cha Nike na ‘pulova’ la raungi nyeusi na ndani ilionekana alikuwa ana kitu kingine cheupe ingawa ilikuwa si lahisi kukijua.

Salehjembe linaamini nguo iliyokuwa ndani ya ‘pulova’ haikuwa ile shati yake, itakuwa ni nguo nyingine mpya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic