May 4, 2013





Bondia Francis Cheka amesema hakuna bondia nchini anayeweza kufanya mazoezi makali kama ambayo amekuwa akiyafanya.

Cheka ambaye siku chache zilizopita alitoa kipigo kikali kwa Thomas Mashali na kumchapa kwa knockout (KO) katika raundi ya 10.

Akizungumza na Salehjembe, Cheka alisema amekuwa akifanya mazoezi makali sana chini ya kocha wake Abdallah Saleh maarufu kama Komando.


“Sidhani kama kuna bondia anaweza kufanya mazoezi kama mimi, ni makali sana na kocha wangu hataki mzaha hata kidogo.

“Nimekuwa nikipanda milima na hauwezi kuamini, kocha wangu anachofanya si kwamba yeye anakaa ananisubiri. Badala yake tunakimbia pamoja.

“Unaweza kudhani anakuwa nyuma, pamoja na kuwa na umri mkubwa yeye ndiye anakuwa mbele na ninalazimika kumfuata.

“Mazoezi yangu ni makali sana, unatakiwa kuwa mvumilivu kweli ili kuyafanya na kumaliza hadi mwisho,” anaelezea Cheka.

Kuhusiana na kuendelea kupambana, Cheka alisema anataka kupumzika kwa muda kabla ya kuendelea kucheza tena.

“Si kwamba nimejiondoa katika ngumi, napumzika tu kama inavyotakiwa kwa bondia. Unajipa muda kidogo baada ya pambano.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic