May 4, 2013




Uongozi wa klabu ya Simba umeanza kusaka kimyakimya kipa mwingine kwa ajili ya kuimarisha kikosi.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya klabu hizo zinaeleza, tayari Simba imeanza kufanya mazungumzo na makipa kadhaa wanaocheza katika timu za Ligi Kuu Bara.


Tayari Simba ina makipa wawili wa kimataifa ambao ni Juma Kaseja ambaye ni nahodha wa Taifa Stars na Abel Dhaira ambaye ni kipa wa timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’.

Uamuzi huo wa Simba unaonekana kuwashtua wengi kwa kuwa kama itasajili kipa mwingine, maana yake kati ya Kaseja au Dhaira mmoja atalazimika kuondoka.

“Uamuzi huu umeishajadiliwa na kamati ya ufundi na suala hilo likapelekwa katika kamati ya usajili, hivyo limeanza kufanyiwa kazi.

“Kidogo hata sisi linatugawanya kidogo kwa kuwa hatujui nani ataendelea kubaki kati ya Kaseja na Dhaira. Maana kama ni makipa hao wangebaki wanatosha sana,” kilieleza chanzo.

Pamoja na kutua kwa Dhaira, lakini Kaseja aliendelea kudaka mechi nyingi zaidi baada ya kuonekana ana kiwango bora zaidi.

Hivi karibuni Simba wamekuwa wakimpa nafasi Dhaira ambaye mashabiki walikuwa wana hamu ya kumuona akicheza.

Huenda wamemchoka Kaseja ambaye alitua Simba mwaka 2002 na kuanza kuichezea mechi za mashindano mwaka 2003. Lakini bado ameendelea kuwa kipa bora zaidi Tanzania Bara kwa kipindi kirefu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic