June 15, 2013



Kikosi cha Ivory Coast kitaondoka mara moja mara baada ya mechi ya Taifa Stars kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Bado haijajulikana kama watarudi tena hotelini Bahari Beach, lakini taarifa zinaeleza baada ya mechi huenda wakaunganisha moja kwa moja hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kuondoka zao.
 
“Kweli baada ya mechi hatutalala Tanzania,” alisema mmoja wa maofisa wa timu hiyo kambini kwao Bahari Beach.

“Huo ndiyo umekuwa uamuzi na tunalazimika kufanya hivyo kwa kuwa tumekuja na ndege ya kukodi ambayo tutandoka nayo.

“Tunaona ni vizuri kufanya hivyo kwa maana ya muda, lakini bado wachezaji wengi wanacheza nje ya Ivory Coast na wangependa kuwahi kurudi katika mapumziko na baadaye kujiunga na timu zao kwa maandalizi ya msimu mpya,” alisema.

Mechi ya kesho inasubiriwa kwa hamu kubwa na Stars inatakiwa kushinda ili kujiweka kwenye njia ya kuendelea kuwania kucheza Kombe la Dunia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic