June 28, 2013




Juhusi za Kocha Mpya wa Man United, David Moyes zimegonga mwamba baada ya Everton kusema haimuuzi beki wake wa kushoto, Leighton Baines.
Everton imeiambia Man United iliyotoa ofa ya pauni milioni 12 kwamba haina mpango wa kumuuza beki huyo.

Moyes aliyejiunga na United akitokea Everton ndiye alikuwa akimtaka beki huyo lakini klabu hiyo imesema hauzwi.


Imeelezwa Kocha Mpya wa Everton, Roberto Martinez naye amesisitiza beki huyo asiondoke ili kujenga kikosi imara zaidi.

Uongozi wa Everton umeishatangaza kwamba unataka kubaki na Baines ambaye anaonekana kumpa shida Ashley Cole katika namba tatu katika kikosi cha timu ya taifa ya England.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic