June 28, 2013




Hispania imefanikiwa kusonga hadi fainali ya Kombe la Mabara baada ya kuifunga Italia kwa mikwaju 7-6 ya penalti.

Mechi hiyo kali ilimalizika kwa mikwaju ya penalti baada ya timu hizo kumaliza dakika 120 bila bao.

Sasa Hispania inakutana na wenyeji Brazil katika mechi ya fainali itakayopigwa kwenye Uwanja wa Maraccana Jumapili.

Katika penalti tano za mwanzo timu zote zilifunga baada ya kila upande ulipata na zilipofika za sita, kila upande ukafunga pia.

Lakini ilipofikia penalty ya saba, Italia wakakosa na Jesus Navas akafunga ya mwisho na kuipa ushindi Hispania.

Awali, mechi hiyo hiyo ilikuwa kali na ya kusisimua na si kama ambavyo ilivyoonekana awali kwamba ingekuwa mchekea kwa mabingwa wa Dunia, Hispania.

Italia ilicheza bila ya mshambuliaji wake nyota, Mario Balotelli na ilionyesha soka la uhakika na kuwapa wakati mgumu Hispania.

Mechi hiyo ilimalizika sare ya bila bao katika dakika 90 na zilipoongezwa dakika 30, bado matokeo yakabaki kuwa hayo.

Timu hizo zikaingia katika mikwaju ya penalti na kabla ya kuanza kupiga, kipa Buffon wa Italia alionekana kulalama ingawa haikujulikana alikuwa akilalama kitu gani.

Mara ya mwisho Hispania kupoteza mechi kwa mikwaju ya penalti ilikuwa mwaka 2002 katika Kombe la Dunia dhidi ya Korea.

Msanii maarufu wa pop, Shakira ambaye alikuwa jukwaani, alikuwa kivutio kila alipoonyesha.

Shakira alikuwa uwanjani hapo kumuunga mkono mpenzi wake Gerard Pique ambaye ni beki wa kati wa Hispania na Barcelona.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic