June 28, 2013



Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga wameamua kuboresha zaidi safu yao ya ulinzi baada ya kumsajili kipa Deo Munishi maarufu kama Dida.

Mmoja wa ‘majembe’ ya Yanga katika suala la usajili, Abdallah Bin Kleb amethibitisha kumsajili Dida.

“Kweli tumemsajili Dida, tumempa mkataba wa miaka miwili na lengo letu ni kuimarisha safu ya ulinzi.


“Hivyo Dida atashirikiana na Barthez kuimarisha ulinzi katika lango la Yanga,” alisema Bin Kleb.

Dida alikuwa kipa wa Azam FC, lakini timu yake hiyo haikumpa mkataba baada ya kuingia katikam mgogoro kutokana na shutuma za kupanga matokeo.

Azam FC ililifikisha suala hilo kwa Taasisi ya Kupamabana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na baada ya muda majibu yalitoka Dida na wenzake Erasto Nyoni, Agrey Morris na Said Morad hawakuwa na hatia.

Kabla ya kutua Azam FC, Dida alikuwa kipa namba moja wa Mtibwa Sugar aliyojiunga nayo akitokea Simba alikokuwa kipa namba tatu chini ya Juma Kaseja na Ally Mustapha ‘Barthez’.

Maana yake Dida amekutana na Barthez kwa mara nyingine tena, safari hii wakiwa makipa wa Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic