June 16, 2013

 
Lamouchi akiwa na Saleh Ally leo asubuhi baada ya mahojiano yao..
Kocha Mkuu wa Ivory Coast, Sabri Lamouchi amesema hawaichukulii kwa utani mechi ya leo kwa kuwa ni kama fainali.

Lakini Kocha wa Stars, Kim Poulsen amesema wanachotaka ni ushindi kwa kuwa wakishindwa leo, basi mechi dhidi ya Gambia itakuwa ni sawa na ya kujifurahisha tu.

“Heshima yetu kwa Tanzania ni kubwa sana, lakini tunajua umuhimu wa mechi hii. Kazi yetu kama wanaume ni kupambana uwanjani na ndicho tutakachofanya,” alisema Lamouchi ambaye ni raia wa Ufaransa mwenye asili ya Tunisia aliyekuwa kiungo nyota katika timu za Ales, Auxerre, Monaco za Ufaransa, Parma na Inter Milan za Italia. Pia timu ya taifa ya Ufaransa.

Lamouchi alikuwa akiwindwa na waandishi kwa kuwa hakutokea katika mkutano wa waandishi, hivyokufanya watu wasipate neno lake kuhusiana na mechi hiyo.

Katika mahojiano hayo, mengine ambayo yatatoka katika gazeti la CHAMPIONI la keshi Jumatatu, Lamouchi pia amemzungumzia mshambuliaji Didier Drogba na beki Kolo Toure.

Kwa upande wa Poulsen alisema mechi ni ngumu kwa kuwa wanacheza na wajuzi lakini kikosi chake kitacheza kama timu.
“Tunajua umuhimu wa ushindi wa leo, kila mmoja anataka kushinda na tunajua hauwezi kupatikana bila ya sisi kushirikiana uwanjani,” alisema Mdenishi huyo.


TAYARI IVORY COAST WAKO NJIANI KUELEKEA TAIFA NA BAADA YA MECHI WATAONDOKA KWENDA KWAO IVORY COAST.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic