June 13, 2013





Kocha wa zamani wa Simba, Patrick Liewig alikuwa hajui kama tayari Ngassa ameishajiunga na Yanga.
Liewig alisema anataka kuwaona wachezaji wake wa zamani akiwemo Ngassa.

Lakini alipoambiwa Ngassa ameshajiunga na Yanga, alionekana kushangazwa na hali hiyo.
“Basi mimi sijui, lakini siwezi kuzuia. Hata kama ameenda lakini vizuri Simba wangembakiza.

“Ukitaka kumsajili mchezaji anayemaliza mkataba, vizuri ufanye naye mazungumzo ndani ya miezi sita.
“Ngassa ni mtu mzima anaweza kuamua anachotaka, lakini ndiyo hivyo,” alisema.

Ngassa alijiunga na Yanga rasmi mara tu baada ya mechi dhidi ya Simba, lakini inaonekana Liewig hakuelewa lolote.

Liewig yuko nchini kudai fedha zake kutoka kwa uongozi wa Simba ambao umeingia mkataba na Abdallah Kibadeni kama kocha mkuu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic