June 24, 2013


 
Simba imeendelea na mikakati ya kukiimarisha kikosi chake ambapo sasa imewasainisha nyota wengine wanne makinda.

Hatua hiyo ya Simba inakuwa ni muendelezo wa kukifanyia marekebisho kikosi chake ambacho hakikufanya vizuri msimu uliopita baada ya kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Bara.
 
Omari
Simba ambayo inaonyesha kuelekeza akili yake katika kusaka nyota makinda, juzi iliwasainisha nyota waliokuwa na kikosi chao cha vijana, mabeki Emily Mgeta na Omari Salum. Pia ilimsainisha nyota wa zamani wa Tanzania Prisons, Sino Agustino ambaye ameonyesha kukubalika kwa mashabiki wa klabu hiyo katika majaribio yaliyofanyika chini ya kocha Abdallah Kibadeni.

Wekundu pia wamemsainisha kiungo mwingine mshambuliaji kinda, Marcel Kaheza.
 
Kaheza..
Akizungumza na Championi Jumatatu mara baada ya zoezi hilo, Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Mzee Kinesi’ alisema kusainishwa kwa nyota hao kumetokana na mapendekezo ya Kibadeni ambaye ameonyesha kuridhishwa na uwezo wa wachezaji hao.

“Tumezingatia mapendekezo ya kocha, kati ya hawa wachezaji wote unaowaona leo yeye (Kibadeni) ndiye aliyetaka tuwape mikataba, bado tunaendelea na usajili kwa kuwa kuna nafasi kama ya mshambuliaji na beki wa kati. Tunaendelea kutafuta nyota sahihi tunaowataka,” alisema Mzee Kinesi.

Awali, Simba iliwasainisha makinda wake wapatao 10 na Championi Jumatatu lilikuwa la kwanza kuandika na kutoa picha zao.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic