June 28, 2013





Timu ya Toto African ya Mwanza imeendelea kuwa katika wakati mgumu kutokana na kukimbiwa na wbaadhi ya wachezaji ikiwa ni muda mfupi baada ya kushuka daraja kutoka Ligi kuu Bara na kutakiwa kucheza Ligi Daraja la Kwanza.

Toto ambayo maskani yake ni jijini Mwanza, imeondokewa na wachezaji wake sita ambao wametua kwenye timu nyingine.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Kocha wa Athumani Bilal ‘Bilo’ alisema wachezaji hao walikuwa tegemeo kwenye kikosi chake wameondoka na anafikiria kingine cha kufanya juu ya mbadala wao.

Amewataja wachezaji walioondoka na timu walizoelekea Peter Mutabuzi (Kagera), Selemani Jingo (Kagera), Erick Muloko, James Madafu (Prison), Musa Said (Kagera) na Simba Boaz aliyejiunga Rhino Rangers.

“Nikiwa kocha kuna kazi ya kuziba mapengo hayo kwa kufanya usajili wa wachezaji wengine ili turejee Ligi Kuu Tanzania Bara,” alisema Bilal ambaye aliongeza kuwa ameshaanza mazoezi na kikosi hicho kwenye Uwanja wa Nyamagana.

SOURCE: CHAMPIONI.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic