June 28, 2013





Kikosi cha Wabunge wa Yanga kitakachocheza mechi katika tamasha la Matumaini litakalofanyika Julai 7 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kimeongeza nguvu.

Kikosi hicho cha Wabunge wa Yanga kitakachovaana na wale wa Simba, kimeongeza nguvu kwa kuwachukua Ally Mustapha ‘Barthez’, Athumani Idd ‘Chuji’, Kelvin Yondani na Mrisho Ngassa.


Maana yake kikosi hicho kitakuwa na nguvu zaidi ya kuhakikisha kinawalaza Simba ambao mwaka jana walishinda kwa mikwaju ya penalty.
Imeelezwa hata Simba pia wanaruhusiwa kuongeza wachezaji kwa idadi kama waliyoongeza Yanga ili kujiimarisha zaidi.

Kikubwa ni timu hizo kuchukua wachezaji kutoka Simba na Yanga kwa lengo la kujiimarisha zaidi na kujiweka safi kabla ya mechi hiyo.

Tayari mechi hiyo ni gumzo kubwa na kila upande umepania kushinda ili kuweka heshima lakini Yanga inataka kushinda lakini pia kulipa kisasi.

Tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka, linajumuisha michezo mbalimbali pamoja na burudani za kila aina zitakazoanzaa siku hiyo ya sabasaba, asubuhi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic