June 27, 2013



Mabeki wa Yanga watakuwa na kazi kubwa ya kupambana na washambuliaji wa hatari wa KCCA ya Uganda.

Yanga na KCCA zitapambana Juni 6 jijini Mwanza katika mechi maalum ya kirafiki kujiandaa na msimu mpya.

Washambuliaji hao, Tony Odur, Herman Wasswa, Gaddafi Kiwanuka na Brian Majwega ndiyo walikuwa tishio kubwa kwa mabaki msimu uliopita katika Ligi Kuu ya Uganda na mwisho waliiwezesha timu yao kubeba ubingwa.

Kikosi cha Ernies Brandts ndicho kilimaliza ligi msimu uliopita kikiwa na mabeki wagumu zaidi kupitika hadi mwisho wa ligi wakaisaidia timu yao kubeba ubingwa.


Maana yake mechi hiyo itakuwa ni ya ushindani mkubwa kutokana na sifa hizo mbili za timu hizo ambao ndiyo mabingwa wa Tanzania Bara na Uganda.

Yanga itacheza mechi mbili dhidi ya KCCA katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na baadaye kwenye Uwanja wa Kambarage katika Manispaa ya Shinyanga mjini.
na timu hizo

awali Yanga walipanga kuweka kambi nchini Uholanzi lakini wakaahirisha kwenda kutokana na kutakiwa kushiriki michuano ya Kagame ambayo hata hivyo walijitoa baadaye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic