Pamoja na Barcelona
kutoaofa ya euro milioni 35 ili kumnasa difenda David Luiz, klabu yake ya
Chelsea imesema hapana.Chelsea imekataa katakata beki wake huyo wa kati kutua Barcelona ambao wamekuwa wamkihaha kupata beki wa uhakika kuziba pengo la Carles Puyol ambaye umri umemtupa mkono.
Barcelona wamekuwa wakihaha kupata beki wa kati wa uhakika kwa kipindi kirefu sasa lakini mambo yanaonekana hayajakamilika.
Barcelona au 'Azulgrana' pia inamtaka Thiago Silver wa PSG ambaye hucheza beki pacha na Luiz katika timu ya taifa ya Brazil.







0 COMMENTS:
Post a Comment