July 13, 2013


AL FAYED, MMILIKI WA ZAMANI WA FULHAM AKIWA KARIBU NA SANAMU LA MICHAEL JACKSON..


Mmiliki mpya wa klabu ya Fulham, bilionea Shahid Khan ameonywa mapema kuwa makini kabla ya kuchukua uamuzi wa kuliondoa sanamu la Michael Jackson.

Sanamu hilo la msanii huyo maarufu zaidi wa Marekani ambaye sasa ni marehemu limewekwa kwenye jengo la Fulham na kulikuwa na taarifa kwamba Khan kutoka Marekani angeweza kulitoa.
 
AL FAYED AKIWA NA KHAN AMBAYE NI MMILIKI MPYA

Pamoja na kuonywa na mashabiki, lakini aliyekuwa mmiliki wake, Mohamed Al Fayed pia amemtaka Khan kuwasilikiza mashabiki kabla ya kuchukua uamuzi.

Amemwambia sanamu hilo waliloliweka mwkaa 2001, ni sawa na mali ya mashabiki na wanataka kushirikishwa kabla ya uamuzi wa kuliondoa.

Fayed, 84  alisema ana uhakika klabu hiyo aliyoiuza kwa pauni milioni 200 imepata mtu sahihi ambaye ataiendeleza vizuri na kufanya mambo kwa ufasaha.

Kwa upande wa Khan naye amesisitiza kwamba atahakikisha anaheshimu historia ya klabu hiyo na kuendeleza mazuri ya Al Fayed aliyeimiliki klabu hiyo kwa miaka 16.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic