July 12, 2013


KIEMBA (KULIA) AKIWA MAZOEZINI SIMBA
Ndoto za kiunyo nyota wa Simba, Amri Kiemba kucheza soka la kulipwa nje ya Tanzania, zimeanza kuingia doa.

Inaonekana timu zilizokuwa zinamtaka kutoka katika nchi za Israel, Ureno na Morocco zimesitisha zoezi hilo na chanzo kimeelezwa kuwa umri.

Timu ya Raja Casablanca ya Morocco ndiyo ilikuwa ikienda kasi kutaka kumnasa Kiemba, lakini mambo yamekuwa tofauti.
Awali timu hiyo ilikuwa tayari kutoa hadi dola 150,000 lakini Simba ikaona ni kiasi kidogo.

Alipoulizwa juu ya taarifa hizo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope alisema imekuwa vigumu kwa mchezaji huyo kuweza kupata timu kirahisi kutokana na umri wake kumtupa mkono.


“Siyo lahisi kupata timu haraka kwa Kiemba kufuatia umri wake kuwa mkubwa, kwani kwa sasa ana miaka 30, hivyo kufanya klabu ziweze kusuasua katika suala zima la kumsajili.

“Kwa sasa bado tunaendelea na maongezi na klabu hizo na iwapo tutafikia makubaliano basi atakwenda,” alisema Hans Pope.

Hivi karibuni, Kiemba alisaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Simba kwa dau la shilingi milioni 35, licha ya kuwa Yanga nayo ilikuwa ikimuwania.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic