July 5, 2013



Shirikisho la Soka Afrika (Caf) limeteua waamuzi kutoka Burundi kuchezesha mechi ya kwanza ya mchujo ya Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (Chan) kati ya Tanzania, Taifa Stars na Uganda, The Cranes itakayofanyika Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao ni Thierry Nkurunziza atakayepuliza filimbi wakati wasaidizi wake watakuwa Jean Claude Birumushahu na Pascal Ndimunzigo. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni pacifique Ndabihawenimana.


Kamishna wa mechi hiyo Gebreyesus Tesfaye kutoka Eritrea. Tesfaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka Eritrea na mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Chan.

The Cranes inanolewa na Kocha Mserbia, Milutin Sredojevic ‘Micho’ aliyewahi kuinoa Yanga na baadaye timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi’.

Wakati huo huo, Shirikisho la Soka Afrika (Caf) limeteua Leslie Liunda wa Tanzania kuwa Kamishna wa mechi kati ya Burundi na Sudan itakayochezwa jijini Bujumbura.

Mechi hiyo ya kwanza ya mchujo ya Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (Chan) itafanyika keshokutwa (Julai 7 mwaka huu). Liunda anatarajia kuondoka leo usiku (Julai 5 mwaka huu) kwenda Bujumbura.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic