July 5, 2013


RAIS KIKWETE AKICHEZA MPIRA NA MGENI WAKE RAIS WA MAREKANI BARACK OBAMA, WIKI ILIYOPITA JIJINI DAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Matumaini ambalo litafanyika kesho Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mbali na kuwa mgeni rasmi, Rais Kikwete ambaye ni mdau mkubwa wa michezo ya soka na kikapu, anatarajiwa kuwa mwamuzi wa mchezo wa soka ambao utawakutanisha Wabunge wa Simba watakaopepetana na wenzao wa Yanga, ikiwa ni sehemu ya tamasha hilo.

Mratibu wa tamasha hilo ambalo linafanyika mara moja kwa mwaka, Abdallah Mrisho amesema kuwa Rais Kikwete amekubali kuwa mgeni rasmi ambapo tachezesha mechi hiyo lakini pia atatoa neno la matumaini mwa maelfu ya watu watakaojitokeza uwanjani hapo.


Akizungumzia zaidi Mrisho anasema: “Rais Kikwete amekubali ombi letu la kuwa mgeni rasmi, pia atashika kipenga na kuchezesha mechi ya Wabunge kwa dakika kadhaa, ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa mechi hiyo ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa.”

Katika tamasha hilo kutakuwa na burudani na michezo mbalimbali ambapo litaanza saa nne asubuhi na kufikia tamati saa sita usiku.

“Mchezo mwingine wa siku hiyo utakuwa kati ya Bongo Fleva dhidi ya Bongo Muvie, burudani nyingine ni pambano la ndondi kati ya mwigizaji Aunt Ezekiel dhidi ya Mbunge Ester Bulaya, staa mwingine wa filamu Jacqueline Wolper atapigana na Mbunge Halima Mdee, Mbunge Zitto Kabwe atachapana na Vincent Kigosi ‘Ray’,” alisema Mrisho na kuendelea:

“Mbali na mapambano hayo ya burudani, kutakuwa na mapambano ya ukweli kati ya Francis Miyeyusho dhidi ya Shadrack Muchanje, Thomas Mashali dhidi ya Patrick Amote.”

Mrisho aliongeza kuwa kutakuwa na burudani ya wanamuziki wengi, baadhi yao ni rapa wa Kenya, Jackson Makini ‘Prezzo na Nasib Abdul ‘Diamond’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic