August 5, 2013


Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni, amesema anahitaji mechi tano za kirafiki kabla ya Ligi Kuu Bara kuanza, baada ya kubaini makosa mbalimbali kwenye kikosi chake.

Simba juzi Jumamosi ilicheza dhidi ya Kombaini ya Polisi, mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kutoka sare ya bao 1-1.
Katika mchezo huo, Simba haikuonyesha uwezo wa kutisha, hali iliyosababisha mashabiki kutamka kuwa, Kibadeni awaachie timu yao.

Akizungumza jijini Dar, Kibadeni alisema timu yake bado haijawa fiti na kabla ya ligi anahitaji mechi tano za kirafiki kwa kuwa amebaini matatizo makubwa kwenye safu ya ulinzi.  

Alisema anahitaji muda zaidi kukijenga kikosi chake kwa kuwa bado hakijaonyesha kuwa imara kwa ajili ya ligi kuu.

“Timu nzuri ila kuna matatizo mbalimbali, hasa kwenye safu ya ulinzi, nafikiri nikipata mechi tano za kirafiki kabla ya ligi, nitakuwa nimepata kikosi bora.

“Bado naendelea kujenga kikosi kwa kushirikiana na benchi langu la ufundi, hatutakiwi kuwa na hofu na timu yetu kwa kuwa muda uliobaki unaweza kubadilisha kila kitu na tutakaa sawa kwenye ligi,” alisema Kibadeni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic