September 28, 2013


Mabingwa Yanga wamejiongezea pointi tatu baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting.


Bao pekee la Yanga lilipatikana katika dakika ya 63 kupitia kwa Hamis Kiiza baada ya kuunganisha krosi safi ya Mrisho Ngassa aliyemtoka Stephano Mwasyika na kupiga krosi safi.

Ngassa aliyekuwa anaicheza Yanga kwa mara ya kwanza msimu huu, mwanzo alionekana tatizo kwa mabeki wa Shooting lakini baadaye walifanikiwa ‘kumtuliza’.

Mechi hiyo ilikuwa na ushindani mkubwa huku Ruvu inayonolewa na Boniface Mkwasa ikicheza soka la kibabe la England huku ikichanganya pasi kama La Liga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic