September 28, 2013


Mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe amesema anataka kufunga mabao zaidi kila atakapopata nafasi, lakini ikitokea ikashindikana, zaidi anapenda kutoa pasi zinazozaa mabao.


Akizungumza jijini Dar, Tambwe raia wa Burundi alisema hakunamchezaji anayeweza kufunga kila kukicha.

“Ili ufunge, wenzako watakupa pasi. Kama imetokea uko katika nafasi hauwezi kufunga, vizuri ukatoa pasi.

“Sifa ya mshambuliaji mzuri ni yule anayefunga lakini pili, yule anayetoa pasi zinazozaa mabao.

“Mnapocheza pamoja mnakuwa timu na lengo ni kuisaidia timu, ndiyo maana unaona sipendi uchoyo, natoa kwa kila aliyekuwa kwenye nafasi ya kufunga. Lakini nikiona naweza kufunga, nafanya hivyo mara moja,” anasema Tambwe.

Tayari Tambwe ana mabao 6 na ndiye anaongoza listi ya wafungaji bora wa Ligi Kuu Bara.

Kesho, Mrundi huyo anashuka dimbani na kikosi cha Msimbazi kuwavaa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic