October 6, 2013

MWENYEKITI WA SIMBA, ISMAIL ADEN RAGE NA KATIBU WAKE, EVODIUS MTAWALA (WOTE KUSHOTO) WAKICHUANA NA KATIBU WA YANGA, LAWRENCE MWALUSAKO (KULIA) NA MJUMBE WA KAMATI YAUTENDAJI YA JANGWANI, MOHAMMED BHINDA KATIKA MCHEZO WA KUVUTA KAMBA, HUKU MANEJA WA KILIMANJARO BIA, GEORGE KAVISHE AKIZIDI KUWAPA MCHECHE KWA KUWA 'MAHELA' HEWANI.




Dar es Salaam: Bia ya Kilimanjaro Premium Lager imeleta msisimko mpya katika utani wa jadi kati ya

mashabiki wa Simba na Yanga nchi nzima kupitia kampeni yake mpya ijulikanayo kama NANI MTANI


JEMBE iliyozinduliwa leo jijini Dar es salaam na itadumu kwa muda wa miezi miwili.



Akiongea kwenye uzinduzi, George Kavishe, Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager amesema NANI MTANI JEMBE itawapa fursa ya aina yake mashabiki wa Simba na Yanga kuonyesha mapenzi yao kwa Simba na Yanga kupitia kampeni hiyo itakayoendeshwa kwa sms ambapo Shilingi milioni 100 zitagawanywa kati ya Simba na Yanga halafu fedha hizo zitawekwa katika benki maalum mtandaoni.







¸ Kama nilivyosema awali, NANI MTANI JEMBE itahusisha mashabiki wa klabu za Simba na Kilimanjaro Premium Lager imetenga kiasi cha shilingi milioni 100 ambazo zitashindaniwa.

¸ Kampeni itakapoanza kila klabu itatengewa kiasi cha shilingi milioni 50.

¸ Katika kipindi hicho chote mteja ambaye ni Mtani Jembe akibandua ganda la kizibo cha Bia ya Kilimanjaro.

¸ Mwisho wa kampeni kama mashabiki wa Simba walipiga kura zaidi na kuichangia zaidi.

¸ Mteja anayetuma SMS atachajiwa kiwango cha kawaida cha kutuma sms na baada ya mwisho wa kampeni fedha hizo zitakabidhiwa kwa uongozi wa kila timu kulingana na matokeo ya

kura na klabu zitajiamulia namna ya kutumia fedha hizo katika miradi yake ya maendeleo.

Kampeni hii inatarajiwa kuongeza chachu ya ushindani kati ya mashabiki wa Simba na Yanga kwa kuwapa fursa kuonyesha mapenzi yao kwa timu zao. 

Mbali na kampeni ya SMS, kutakuwepo na shilingi milioni 2 ambazo mashabiki watajishindia kila wiki kwa wiki kumi kwa mashabiki watakaoshiriki zaidi. Vilevile Nani Mtani Jembe itawaburudisha mashabiki wa Simba na Yanga kupitia matukio mbalimbali mabonanza, promosheni zitakazofanyika barabarani, kwenye bar na kwenye matawi ya Simba na Yanga.

 Kampeni hii itafika kileleni tarehe 14 Disemba 2013 ambapo mechi ya hisani itachezwa kati ya klabu hizo mbili kwenye Uwanja wa Taifa mbele ya maelfu ya mashabiki wa timu hizo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic