November 22, 2013





Mwenyekiti wa Simba aliyesimamishwa, Ismail Aden Rage amerejea nchini na kuahidi kumwaga ugali kwa kuwa waliomsimamisha wamemwaga mboga.
 
Rage amerejea nchini Saa 1 na ushee usiku akitokea nchini Sudan na kusisitiza kwamba atazungumza kesho saa saba mchana kwenye makao makuu ya klabu hiyo.
MASHABIKI WACHACHE WALIOJITOKEZA KUMPOKEA

Rage alipokelewa na mashabiki wapatao 120 waliokuwa katika mabasi matatu ya kukodi, ambao walikuwa wakiimba nyimbo za kuonyesha wamekwenda kumpokea.
AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI

Hata hivyo ilionekana wazi mashabiki hao wengi hawakuwa wanachama wa Simba, na idadi yao haikuwa kubwa kama ambavyo ilitarajiwa awali.

Baada ya kutoka alizungumza na waandishi wa habari halafu akaingia kwenye gari aina ya Toyota na kuondoka zake hadi klabu ambako alitoa ahadi hiyo ya kumwaga ugali kesho.

Rage alisimamishwa kwa madai ya kutoshirikiana na viongozi wenzake ikiwemo kamati ya utendaji na maamuzi ya mambo mengi alikuwa akifanya mwenyewe.

Pamoja na hivyo suala la kumuuza mshambuliaji Emmanuel Okwi kwa Etoile du Sahel ya Tunisia, hadi leo Simba inadai dola 300,000 na haijalipwa kitu.

Lakini aliingia mkataba na Azam TV ili Simba TV iwe inaonyeshwa na kulipwa Sh milioni 330 kwa miaka mitatu ikiwa na maana kila mwaka Simba itapata Sh milioni 110, wakati kampuni ya Zuku ilikuwa tayari kutoa dola 300,000 kwa mwaka na walikuwa bado kwenye mazungumzo.
PICHA: LENZI YA MICHEZO

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic