December 17, 2013



 
AMROUCHE AKIWA NA RAIS KENYATTA, IKULU JIJINI NAIROBI
Wakati Adel Amrouche akitangazwa kuwa kocha bora wa michuano ya Chalenji iliyomalizika hivi karibuni nchini Kenya, Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye alisema timu yake ilionekana ni wasindikizaji.
 
Musonye alisema kamati ya ufundi ya Cecafa imemteua Amrouche kuwa kocha bora wa michuano ya Chalenji kutokana na kuwa na timu ambayo iliaminika haiwezi hata kufika fainali.
“Lakini imefika fainali na hatimaye imetwaa kombe,” alisema Musonye.
WACHEZAJI WA HARAMBEE STARS WAKIMBEBA JUUJUU BAADA YA KUTWAA KOMBE

Kabla ya hapo, Amrouche raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria alikuwa kocha wa timu ya taifa ya Burundi na ilikuwa ikifanya vema pamoja na kuandamwa na ukata.
Lakini amekuwa akionyesha uwezo mkubwa, sawa na alivyosema Musonye kwamba timu yake ilionekana haina lolote.
AKIKABIDHIWA TUZO YA KOCHA BORA

Lakini uchezaji wa Harambee Stars katika michuano hiyo pamoja na kwamba haikuwa na wachezaji wenye majina makubwa sana ulikuwa ni wa kiwango cha juu.
Mfano mzuri ilipokutana na Tanzania Bara katika nusu fainali, Kenya ilitawala sana na hasa kipindi cha kwanza.

Lakini Amrouche anayesifiwa kwa uwezo mkubwa wa mipango, aliweka mbinu bora za kuwabana Mrisho Ngassa na Mbwana Samatta na kweli akafanikiwa kuilaza Kili Stars bao 1-0 akasonga fainali.
Bado wengi hawakuipa nafasi timu hiyo, lakini ikaifunga Sudan mabao 2-0 na kufanikiwa kutwaa kombe hilo lililokosekana Kenya kwa zaidi ya miaka saba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic