December 18, 2013





Siku chache baada ya kuachana na Ashanti United, kipa mzoefu Amani Simba ameibuka na kutangaza kuachana na soka rasmi.
Wiki iliyopita Ashanti iliachana na wachezaji wake watano kuelekea kwenye mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, akiwemo kipa huyo.


Ofisa habari wa timu hiyo, Marijani Rajabu, amesema kipa huyo aliuandikia uongozi wa timu hiyo barua ya kuacha kazi siku chache mara baada ya mzunguko wa kwanza kumalizika ambapo uongozi ulipitisha ombi hilo.

Amani aliyeanza kucheza soka la ushindani tangu mwaka 1998, amesema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa anahitaji kupumzika na kuwaachia vijana waonekane na kukuza vipaji vyao kwenye soka.

“Dah, nimecheza sana tangu mwaka 1998, nafikiri muda wangu wa kupumzika na kuwaachia wengine umefika, wapo vijana wengi wanahitaji kuonekana kwa hiyo inabidi tuwapishe nao pia waonyeshe uwezo wao,” alisema Amani na kuongeza:
“Mimi tena sasa hivi soka langu na timu zangu zitakuwa za maveterani, niliandika barua ya kuacha kazi Ashanti ni kwa sababu hii na wala si nyingine kama watu wanavyodhani.”
Amani ameshachezea jumla ya timu tisa katika ligi kuu mpaka sasa ambazo ni Tanzania Prisons, Moro United, Polisi Moro, Mtibwa Sugar, Simba SC, Kagera Sugar, JKT Ruvu, Mbeya City na Ashanti United.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic