January 18, 2014


Wakati Yanga inashuka leo dimani kucheza mechi ya kirafiki, Kocha Hans van Der Pluijm amewataka wachezaji wake wauchezee mpira.


Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto amesema kocha huyo mpya amewataka wachezaji kuuchezea zaidi mpira.
“Amewataka kujiamini na kuuchezea mpira lakini kwa malengo. Kocha ameonekana kuwaamini wachezaji.
“Kikosi kimefurahisha, hivyo anachotaka ni wao kujiamini na kuuchezea mpira.
“Tayari ameanza mazoezi na ukweli wachezaji wanaonekana kuyakubali na ukumbuke walianza vizuri na mazoezi pia mazuri kutoka kwa Kocha Mkwasa,” alisema.

Yanga iko kambini Uturuki kwa wiki mbili na tayari imecheza mechi mbili za kirafiki na kushinda zote.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic