Young Africans kesho itashuka dimbani kucheza na timu ya KS
Flamurtari Vlore inayoshika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini
Albania ikiwa ni sehemu ya mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu kwa timu zote,
mchezo utakaofanyika katika eneo la Side Manavagat nje kidogo ya mji wa Antalya nchini Uturuki.
Yanga imeweka kambi ya wiki mbili nchini Uturuki kujiandaa na Ligi Kuu Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika.
Tayari imeshuka dimbani mara mbili na kucheza mechi za kirafiki na zote imeshinda kwa mabao 3-1 na 2-0.









0 COMMENTS:
Post a Comment