January 26, 2014


Baada ya Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic kutua Uwanja wa Taifa jijini Dar, jana kuishuhudia Yanga ikicheza na Ashanti United, leo wa Yanga naye amejibu mapigo.

Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm naye ametua uwanjani hapo na kuishuhudia Simba ikivaana na Rhino ya Tabora na kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
Pluijm alitua uwanjani hapo akiwa na Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh ambaye alikuwa akimpa mambo kadhaa aliyotaka kujua kuhusiana na kikosi cha watani wake hao Simba.
Kocha huyo raia wa Uholanzi, hiyo ilikuwa mara yake ya pili kuingia Taifa baada ya jana kuingia kwa mara ya kwanza na kuingoza Yanga kuishinda kwa mabao 2-1.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic