January 27, 2014


Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi, amesema siri ya ushindi kwenye mechi yao dhidi ya Kagera Sugar ni kujituma kwa wachezaji wake pamoja na kufuata maelekezo yake.
 
Mbeya City ambayo inaendelea kuzitesa timu za Ligi Kuu Bara, juzi Jumamosi iliifunga Kagera Sugar bao 1-0 ugenini kwenye Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera na kuzidi kuwapumulia vinara Yanga kwa tofauti ya pointi moja.

 Mwambusi amesema baada ya kutoka kwenye michuano ya Mapinduzi ambayo kikosi chake hakikufanya vizuri, aliwapanga upya vijana wake na kuanza maandalizi kwa kuufanyia kazi upungufu uliojitokeza kwenye michuano hiyo.
Alisema pia anawapongeza mabeki wa timu zote kwa kuwa walifanya kazi ya ziada kuwazuia washambuliaji wa timu zote lakini zaidi wa Mbeya city ambao wanaonekana kuimarika.
Aliongeza kuwa mechi yao dhidi ya Ruvu itakayochezwa keshokutwa Jumatano, itakuwa ngumu na matokeo yatapatikana ndani ya dakika 90.
“Siri ya ushindi ni maandalizi mazuri, pia Kagera walikuwa vizuri lakini zaidi pongezi kwa mabeki wa timu zote kwa kuwa walifanya sana kazi ya kuzuia.
“Mechi yetu na Ruvu siwezi kusema tutashinda au la, tambua mimi naheshimu timu zote, kwa hiyo matokeo ni dakika 90 na nitayapokea yoyote,” alisema Mwambusi.  


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic